Jifunze maarifa mbalimbali ya kiroho na kimwili,tambua ulimwengu wa kiroho hasi na chanya,elimu zilizofichwa,zijue dawa na nguvu za asili za miujiza na utendaji wake. Call us +255 675 841177 email monicajonathan2000@gmail.com

Total Pageviews

Search

Tuesday, June 27, 2023

Je ni kweli waafrika tulikuwa tunavaa ngozi za wanyama na kuishi mapangoni?

Leo nataka tujifunze kitu na katika kitu muhimu ambacho unatakiwa kufundisha hata mwanao basi ni hiki cha leo maana kitamfanya asiishi kwenye giza Leo nimewasogezea bi.dada huyu hapa anaitwa TIYE(Tye,Taia,Tiy,Tiyi) huyu ni BIBI yetu aliishi miaka ya 1338 BC na alikua ni mke wa farao AMENHOTEP III(wa tatu) na mtoto wao waliomzaa alikua Farao AKHENATEN hivyo yeye ndiye BIBI wa farao TUTANKAMUN Yani huyu alikua ni Malkia(queen) mke wa farao AMENHOTEP na MAMA yake alikua akiitwa THUYU(Tyuju) BABA yake alikua akiitwa YUYA Sasa tusimchambue sana huyu bibi kwakuwa babu zetu kwenye kuifadhi historia wapo vizuri tunaweza kufika mpaka kizazi cha 5 na tusimalize chimbuko lake yani babu zetu walikua hawana dogo kwenye kutunza historia walijua wajukuu zao ipo siku zitatufaa kama hivi leo Sasa wakoloni na elimu yetu ya mchongo ya shuleni wanatuaminisha kuwa sisi tulikuwa tunaishi mapangoni na tulikua tunavaa mangozi ya wanyama kabla ya kuja wao yani wao ndo waliotuletea nguo na ustaarabu,sasa naomba tuangalie hio sanamu vizuri ya BIBI yetu malkia TIYE tuangalie kwa umakini sana katika yafuatayo. ANGALIA HAIR STYLE YANI MTINDO NA UMARIDADI WA ALIVYOWEKA NYWELE ANGALIA NA HILO VAZI. YANI NI GAUNI FLANI KALI SANA sasa baada ya kuyaona hayo nakuachia kazi wewe mwenyewe jifikilie mavazi walikuwa wanayatoa wapi nani aliekua akiwapima na kuwashonea nani alikua designer(mwanamitindo) wao NOTE;Tupo tunafundishana kutumia akili kabla ya kuamini. Tupo hapa ili kuwatua mzigo wa ujinga uliowekwa na wakoloni katika kichwa chako. kupitia T'CHALLA na wakush wote tutaakikisha una FIKIRI kile unacho takiwa KUFIKIRI na sio KUFIKIRI kile wanachotaka UFIKILI HOTEP HOTEP HOTEP mwisho wa kumnukuu mkushi anayejulikana kwa jina la T'challa Sut'eh kutoka Dsm Tanzania