Leo nataka tuzungumzie chale za wachawi,si ulishawahi kuona,kujikuta ama hata kusikia mtu ameamka amejikuta amechanjwachanjwa na kiwembe?ndyo hizo
CHALE ZA WANGA.
Wanga hushirikiana na jini cheketu katika kukupiga chale na kukujaza nuksi mwilini,pia kila utakapoenda wawe wanakuona mtu wao.
aina za chale za wanga
1.chale za wanga wanaotaka kukufanya msukule
2.chale za kukukaribisha kwenye vikao vyao vya kichawi
3.chale za kukujulisha kwa wachawi kuwa wazazi/wazee wako wewe pia ni wachawi
4.chale za kuiba kivuli chako kitumike kwenye uchawi uonekane wewe mchawi
5.chale za mchawi mwenyewe zinamjulisha kwa wachawi wenzie kuwa ni mwenzao
wachawi wakikupiga chale zao kila chale ina maana yake waliyokusudia lakini kiujumla lazima
(1)Mambo yako kuwa magumu
(2)kujikuta umekatwa katwa mwilini wakati jana ulipoenda kulala ulikuwa safi
(2)kila ikifikaa saa 7mpaka 8usiku lazima ushituke
(3)utasingiziwa unawaroga watu mtaani kwenu
(4)utachukiwa na kuambiwa unaringa wakati kiuhalisia haupo hivyo
ukiona hivyo jua kwamba wanga wamekupiga chale ambazo huwa kama muhuri popote uendapo utajulikana kwa chale hizo
NJIA ZA KUFUTA CHALE ZA WANGA
( 1 ) Chukua kijiti cha wahenga
(2)Chukua fagio lilILotupwa
(3)Chukua sembe umeme
( 4) sembe mangube
(5)usila wa mti ulokufa wenyewe
(6)usila wa mti ulopigwa na radi
(7)sembe Makata
Mfute aliyepigwa chale kuanzia paji la uso
hapo wanga hawatomuweza kumuona kwenye chombo chao
KUJIKINGA NA JINI HUYU WA KICHAWI
Soma sura hizi za kuran wakati unataka kulala hali ya kuwa pumzi yako inayotoka mdomoni inagonga kwenye viganja vyako vya mikono ulivyovikutanisha pamoja
Soma surat ikhlaasw x 7
soma Surat nnaas x7
soma surat lfalaq x7
soma surat fatha na usome ayaturkursiyyux 7
kisha soma dua ya kulala na ujifute mwili wako wote kwa viganja hivyo kasoro sehemu za siri na chini ya nyayo za miguu.
na kwa mtu wa dini nyingine utaomba sala ya kulala kama ilivyo katika imani yako
